Saturday 27 November 2010
Friday 19 November 2010
We are back
We arrived on Friday at about 1623 with Oman Air and went straight to Kempisky for a concert, for our friends who were celebrating their sixth year in marriage. A lot of drinking food and dancing. Saturday kama kazi palepale Salender Bridge Club
Wednesday 17 November 2010
Show ya Njenje Muscat PDO
Tulianza matayarisho saa nne asubuhi onyesho lilianza saa mbili usiku na kuisha saa nane usiku, kuna wapenzi wengi wa Njenje Muscat, Kiswahili utadhani uko Kariakoo
kuwasili asubuhi |
Matayarisho |
Vyombo vilikuwa na tatizo mixer ilikuwa ndogo kuliko tunayotumia kwa kawaida |
Jioni |
gere mama yanguuuueeeeeeeeee |
JFK na Nyota |
raha ndani ya roho |
Babu Njenje ndani ya Conga |
Tuesday 16 November 2010
Njenje usiku wa Idd Muscat
Siku ya Idd Mosi ilikuwa siku yenye kuleta faraja nyingi kwa wanamuziki wa Kilimanjaro Band. Tuliweza kutembelea bendi mbili kati ya tatu zinazotoka Tanzania ambazo ziko hapa Muscat. Jambo lililoleta faraja kubwa ni kukuta bendi hizo zikipiga nyimbo kadhaa za Njenje na tena kwa ufasaha mkubwa. Faraja ilikuwa ni ya aina mbili, kwanza kuwa tungo zetu nyingine za miaka mingi bado zinapendwa, na jingine ni kuwa kuna vijana wa Kitanzania wanaendeleza kwa ufasaha gurudumu letu. Tulijisikia tumepwa heshima kubwa na wanamuziki hawa kwa kuona kuwa kwa kupiga nyimbo zetu waliona kuwa wanapiga kitu kizuri katika show zao. Tulipokelewa vizuri, na kati ya maneno ambayo yalifurahisha ni ya mtoto wa mwanamuziki Hamza Kalala, ambae hujitambulisha kama Totoo Kalala aliyesema, " Wazee endeleeni kutunga ili tuwaige nasi tuweze kula".
Monday 15 November 2010
Njenje wawasili Muscat
Keppy na Waziri safari ya kwenda lunch
Katika safari ambayo ilikuwa ianze Jumanne tarehe 16, ghafla taarifa ilikuja kuwa safari ni Jumapili tarehe 14, na hivyo bendi ikalazimu kuharakisha ratiba zake kuwa mwaliko huo. Na sasa kundi zima la Njenje liko Muscat Oman tayari kwa onyesho tarehe 17 jumatano katika ukumbi wa PDO.
Nje ya apartments tulizofikia |
Stage ambapo litazungushwa duara |
Milima ya huku mimea ni adimu, jua kali mawe kwa wingiii |
Nyota na Abou wakitunga nyimbo mpya |
Ngoja nile byeeeee |
Friday 12 November 2010
Mazoezini wiki hii
Mazoezini, haya mazoezi yalikuwa ya ghafla sana, kuna mtu alipata wazo la nyimbo tukapigiana simu na kukutana na kuanza kutengeneza kitu. Ilikuwa raha
Subscribe to:
Posts (Atom)