Monday 30 May 2011

Lohhh waimbaji wapo wengi


Mduara ulizunguka kama kawaida, lakini pamoja na hayo Jumamosi hii walijitokeza chipukizi wawili na kuimba sawasawa na vizuri kabisa nyimbo mojawapo inayopigwa na bendi. Kwa kweli vipaji jamani vipo.

Thursday 26 May 2011

Leo ni Ijumaa

 
Leo ni Ijumaa, Waziri akiwa tayari kutimiza aliyoagizwa.

Sherehe za kufunga Mkutano wa 6 wa Kimataifa wa Mwasiliano- ICT

 Njenje walikuwepo katika kutoa burudani ya kufunga mkutano huo katika eneo la Mlimani City Alhamisi  may 26.
Babu Njenje(Vocals), Waziri(Keyboards), Abou(Percussion), Juma Omary(Electronic Drums)

Mduara wenye ngongoti



Mduara wenye mtizamo wa Kimataifa


Wednesday 25 May 2011

Njenje wapata ugeni wa K Mondo Sound

Mara kwa mara wanamuziki mbalimbali hutembelea maonyesho ya Kilimanjaro band, week-end hii wageni walikuwa bendi nzima ya K Mondo Sound wazee wa Kibajaj, ambao huwa na onyesho lao kila Ijumaa katika ukumbi wa Triz Motel Mbezi, walileta raha katika ukumbi wa Salender Bridge chini ya uongozi wa Mangustino









Monday 23 May 2011

Nyonga za Arusha zinadhihirisha Tanzania ni moja


Arusha to Dar es Salaam kupitia Kipingu Mgahawa


Baada ya Kilimanjaro Band kutumbuiza katika sherehe ya mkutano wa muungano wa Masecretary TAPSEA siku ya Ijumaa 20 May 2011, bendi ililazimika kuondoka alfajiri ya Jumamosi kuwahi onyesho la kawaida Salender Bridge Club. Safari ilienda salama mpaka tulipokaribia Korogwe ambapo barabara imeharibika kwa kuwa na mashimo mengi. Wakati wa kukwepa sehemu fulani yenye mashimo ya namna hiyo bus moja lililokuwa nyuma yetu likija spidi kali sana lilitaka kuigonga gari yetu kwa nyuma na ikalazimika dereva wetu Waziri Ally ‘Kissinger’, ajitahidi kulikwepa kwa kulazimika kuingia katika mashimo hayo gari letu lilipata pacha mbili kwa mpigo katika matairi ya upande wa kushoto. Babu Njenje aliondoka na gari lililokuwa limebeba vyombo vyetu na kwenda Korogwe mjini kutengeneza tairi hizo. Katika sehemu hiyo tulikuta mgahawa, KIPINGU MGAHAWA’ (hatuna uhakika kama ni mradi wa mwalimu Kipingu), ambao ulikuwa na chapatti safi sana, mama mmoja alikuwa akitengeneza chapatti fresh na tulizipata kwa chai ya rangi taamu. Tuliendelea na safari na kufika Dar salama.
 


Chai chapati Keppy na Nyota

Chai ya rangi



Abuu na Nyota

Pancha tairi mbili

Mkutano , tunafanya nini

Sunday 22 May 2011

NJenje Arusha

Ijumaa 20 May  wanachama wa TAPSEA walipata nafasi ya kupata burudani toka kwa Kilimanjaro Band, katika ukumbi wa AICC Arusha.  Mduara ulipigwa na nyonga zikazungushwa. Tena kulikuwa na kila design ya nyonga hapa.


Kibonde alikuweko

Moddy, Abou, Babu Njenje wakisubiri

Duara linazunguka na nyonga kwa sana

Wenyewe wanaaiita Ekutiiiii

Nyota

Waziri na nyota


Nyota akutana aliyefanana nae

Wednesday 18 May 2011

Njenje kuwa Arusha Ijumaa 20 May, Private Function

Bendi yenu ya Kilimanjaro Band itakuwa Arusha Ijumaa 20 May 2011, kwa show ya siku moja katika 'private function '. Jumamosi jukwaani Salender Bridge as usual duara litazunguka, nyonga zitanyongwa. Kuna uwezekano mkubwa sana mpenzi maarufu wa Kilimanjaro Band Carl akatoa show kali ya nyonga......................

Sunday 15 May 2011

Kachiri kachiri


Jumamosi Njenje raha tele kukosa ni kosa

Kitime wa Man U, Waziri wa Njenje, Babu Njenje

Mgongo huu ni wa Musa Masharubu


Khaleed na filimbi!!!!!!!!


Keppy Kiombile on Bass, Kanku Kelly the master trumpetist

Mjomba Mgaikivembo, akiwa na Palmena Mahalu katika keyboards

Raha ndani ya roho

Modddyyyyyyy

Lily na rafiki

Mzee wa Arsenal na mwandani

Bi Kinyau and Babu Kinyau mmeona nini?


Kidole hichooooooo

Saturday 14 May 2011

Waziri wa Habari Utamaduni na Michezo kukutana wasanii




Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dr. Emmanuel Nchimbi (Mb), atakutana na wasanii katika ukumbi wa BASATA kuanzia tarehe 17 Mei na tarehe 18 Mei, 2011. Waziri ataongea na wasanii kwa utaratibu ufuatao:-

17/05/2011 (Jumanne) Saa 4:00 asubuhi
Wasanii Wote wa Sanaa za Muziki

18/05/2011 (Jumatano) Saa 4:00 asubuhi
Wasanii Wote wa Sanaa za Ufundi,Filamu na Maonyesho




Izingatiwe kwamba Waziri ataongea na wasanii wa muziki wa aina zote wakiwemo wa Kizazi kipya,Bendi,Disco, Asili,Taarab na kadhalika katika siku ya kwanza.Katika siku ya pili yaani Tarehe 18/05/2011 ataongea na wasanii wa Sanaa za Filamu,Maonyesho na Ufundi pekee. Wasanii Wote mnaombwa kujitokeza kwa wingi.
Lengo kuu la mikutano hii kati ya Waziri na Wasanii ni kuongelea maendeleo ya fani za sanaa.






MAZOEZI YA ALBUM MPYA

MAZOEZI KWA AJILI YA ALBUM MPYA YANAENDELE KWA NGUVU SANA

ON STAGE

ON STAGE
ON STAGE

TUNAANZA MWAKA NA NGUVU MPYA