Kilimanjaro Band ni bendi kongwe lakini ni wazi haioni tabu kufanya
kazi mpya, mwaka 2005 bendi ilishirikiana na wanamuziki wa Bongoflava
kutoka Tanga na kufanya onyesho mjini Tanga. Bendi ilifanya mazoezi
nyimbo za wasanii wa Tanga na kuwezesha live performance ya kazi zao.
Kwa mara nyingine tena band itakuwa na show kubwa karibuni, na kwa
wakati huu iko katika mazoezi makali na wanamuziki kadhaa wakiongozwa na
MwanaFA jana waliweza kuonjesha wapenzi wa Njenje kitu gani wategemee
baada ya kufanya onyesho la wasanii hao wakiwemo Mandojo, Domokaya,
MwanaFA, Aboubakry Mzuri, Supper Sele. Kwa upande mwingine mtoto wa
mwanamuziki nguli Mzee Shem Karenga nae alipanda jukwaani na kushika
gitaa na kulipiga kuonyesha karithi kipaji cha baba yake. Picha hapo chini
Ni raha sana jmos keep it up
ReplyDelete