Thursday 7 October 2010

Mwanzo wa Bendi



Kwenye miaka ya sabini kundi la vijana mjini Tanga walianzisha bendi wakajiita The Love Bugs, kundi hili lilikuwa  mchanganyiko wa Magoa na Waafrika, hususan likawa  linapiga nyimbo za wanamuziki wengine hasa kutoka Ulaya na Marekani, baada ya muda vijana hawa wakabadili jina na kujiita the Revolutions na kuhamia Dar Es Salaam. ambapo waliweza kujiweka katika nafasi ya juu kwa bendi zilizokuwa zikipiga mahotelini kwa wakati ule. The Revolutions waliweza kupiga katika hoteli kubwa mbalimbali katika miji ya Arusha and Dar es Salaam. Mwaka  1989 bendi ilienda London kwa mara ya kwanza na huko ikabadilisha jina na kujiita Kilimanjaro Band,wakati ikiwa huko bendi ilitoa album yake ya kwanza‘Kata kata”. Album yenye nyimbo mchanganyiko wa mahadhi na pia lugha. Kata kata wenyewe ulikuwa ni wimbo wa Kiingereza.Katika album hiyo pia ndiyo ulirekodiwa wimbo Njenje ambao umekuwa ukipendwa hadi leo na pia kusababisha bendi hii kuitwa Wananjenje

No comments:

Post a Comment

ON STAGE

ON STAGE
ON STAGE

TUNAANZA MWAKA NA NGUVU MPYA