Sunday 20 August 2017
MSIBA MKUBWA NJENJE
MWEKA HAZINA wa miaka mingi wa Kilimanjaro Band, ambaye alijulikana kwa wapenzi wengi kutokana na kuwa mkata tiketi wa bendi wa miaka mingi sana, Francis Mnguto, maarufu kwa jina la Babu Francis amefariki leo alfajiri nyumbani kwake Ilala Flats Dar es Salaam. Kwa miezi kadhaa Babu Francis amekuwa akisumbuliwa na tatizo la figo. Taarifa kutoka kwa familia ni kuwa mazishi yatakuwa Dar es Salaam Jumatano 23 Agosti. Msiba upo nyumbani kwake Ilala Flats Dar es Salaam.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment