Monday 29 August 2022

WANAMUZIKI WATATU WAJIUNGA NA KILIMANJARO BAND

 

KUMBURU

Baada ya kifo ya Waziri Ally, kiongozi na mpiga kinanda wa Kilimanjaro Band, bendi ilipata pigo kubwa ambalo limechukua muda mrefu kupata ahueni.
 Ili kuendeleza bendi hii kongwe  iliyoanza mwanzoni mwa miaka ya 70 kule Tanga, wanamuziki wapya watatu wamejiunga na kuanza mazoezi makali na bendi hii.
 Kwanza kabisa kuna mkongwe Geophrey Kumburu, huyu ni mpiga kinanda wa miaka mingi ambaye kati ya bendi alizopitia ni Kilimanjaro Connection, MK Group, Vijana Jazz band,Wahenga band, JFK Band na kwa miaka mingi alikuwa akifanya kazi peke yake ikiwemo kuendesha  na studio ya kurekodi muziki. Na kufundisha muziki. Geophrey pia ni muimbaji na ndie amechukua jukumu la kupiga kinanda katika bendi hii kongwe. Pia kuna vijana wadogo wawili ambao ni waimbaji, Martha na Feisal ambao ni wazi uwezo wao uko juu na utaleta nmchango mkubwa katika Kilimanjaro band.

No comments:

Post a Comment

ON STAGE

ON STAGE
ON STAGE

TUNAANZA MWAKA NA NGUVU MPYA